Bernardino wa Siena (8 Septemba, 1380 - 20 Mei, 1444) alikuwa mtawa wa shirika la Ndugu Wadogo na kasisi wa Kanisa Katoliki.
Alizaliwa na kubatizwa Massa Marittima (Siena) tarehe 8 Septemba 1380 katika
familia Albizzeschi kutoka Siena, ambako alihamia baada ya
kubaki yatima, ili alelewe na ndugu zake na
kusomeshwa.
Wito na utume
Akiwa na miaka 22, alijiunga na utawa,
katika tawi la urekebisho wa Waobservanti, ambalo akawa nguzo yake kuu,
pamoja na Yohane wa Kapestrano, Yakobo wa Marka na Alberto wa Sarteano.
Kisha
akaanza utume mkubwa akihubiri kwa mafanikio katika Italia Kaskazini. Kazi
yake yaliamsha katika Kanisa imani na ibada kwa Jina la Yesu na kurekebisha maadili ya wengi. Ndiye aliyesambaza kila
mahali vibao vyenye kifupisho JHS (Jesus
Hominum Salvator) kikiwa na msalaba juu yake na kuzungukwa na jua lenye miali 12.
Kifo
Alifariki
huko L'Aquila, tarehe 20 Mei 1444.

No comments:
Post a Comment