Tuesday, 19 April 2016

Huduma kwa wazee na wagonjwa

Huduma kwa wazee na wagonjwa (Weekend Ministry) Huduma kwa wazee na wagonjwa inatolewa kila Jumamosi saa 4 asbh hadi saa 11 jioni katika viwanja vya parokia ya Segerea. Ni wajibu wetu kuwalea na kuwatunza wazee wetu kadiri neno la Mungu linavyotuagiza. “…………….Katika neno na katika tendo, umheshimu baba yako, ili baraka zote zikujie kutoka kwake. Mradi Baraka ya Baba itaziimarisha nyumba zao watoto, bali laana ya mama huing’oa misingi. ……….. Mwanangu, umsaidie baba yako katika uzee wake, wala usipate kumhuzunisha siku zote za maisha yake. Akiwa amepungukiwa na ufahamu umwie kwa upole, wala usimdharau iwapo wewe u mzima sana; kwa maana sadaka apewayo baba haitasahauliwa, na badala ya dhambi, itahesabiwa kwa kukuthibitisha”. (YBS 3:1-14) Pia kwa habari ya wagonjwa na wenye shida mbalimbali, neno la Mungu linatuhimiza kuwa, “Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya; watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya” (Mk. 16:17-18). Wazee wote, wagonjwa na wenye shida na mahitaji mbalimbali wataombewa. Waamini wote mnakaribishwa

No comments:

Post a Comment