Ni Muungano wa Familia za Kikristo za Kikatoliki kwa Ujirani wao Kuanzia Familia Mbili hadi Kumi na Mbili zinazokutana pamoja angalau mara moja kwa wiki kwa muda wa saa moja kushirikiana katika kusali, kusoma Neno la MUNGU na kulitafakari pamoja kujadili na kushirikiana katika mambo mbalimbali ya kijamii na kiuchumi kulingana na mazingira yao kwa madhumuni ya kumtafakari MUNGU na kuuishi ukristo wao kivitendo ili kuwa watakatifu.
Tuesday, 19 April 2016
Huduma kwa wazee na wagonjwa
Huduma kwa wazee na wagonjwa (Weekend Ministry)
Huduma kwa wazee na wagonjwa inatolewa kila Jumamosi saa 4 asbh hadi saa 11 jioni katika
viwanja vya parokia ya Segerea. Ni wajibu wetu kuwalea na kuwatunza wazee wetu kadiri neno
la Mungu linavyotuagiza. “…………….Katika neno na katika tendo, umheshimu baba yako, ili
baraka zote zikujie kutoka kwake. Mradi Baraka ya Baba itaziimarisha nyumba zao watoto, bali
laana ya mama huing’oa misingi. ……….. Mwanangu, umsaidie baba yako katika uzee wake, wala
usipate kumhuzunisha siku zote za maisha yake. Akiwa amepungukiwa na ufahamu umwie kwa
upole, wala usimdharau iwapo wewe u mzima sana; kwa maana sadaka apewayo baba
haitasahauliwa, na badala ya dhambi, itahesabiwa kwa kukuthibitisha”. (YBS 3:1-14)
Pia kwa habari ya wagonjwa na wenye shida mbalimbali, neno la Mungu linatuhimiza kuwa, “Na
ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha
mpya; watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka
mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya” (Mk. 16:17-18). Wazee wote, wagonjwa na
wenye shida na mahitaji mbalimbali wataombewa. Waamini wote mnakaribishwa
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment